Subscribe:

Ads 468x60px

August 03, 2012

Ngassa Rasmi Simba

Mchezaji aliyesajiliwa kwa mkopo na Simba kutoka Azam, Mrisho Khalfan Ngassa, leo ametambulishwa rasmi kwa wachezaji wenzake na viongozi ikiwa ni pamoja na kukabidhiwa Milioni 30, Gari pamoja na jezi namba 16, aliyokuwa akivaa Azam lakini safari hii ikiwa nyekundu inayomilikiwa na wekundu wa Msimbazi, Simba.
Sakata la Ngassa lilizua gumzo siku mbili hizi kabla ya uongozi wa Simba kumuweka chini na kumalizana naye.
Awali, Ngassa alifanya mazoezi na wachezaji wenzake kwenye fukwe za Coco, Dar-Es-Salaam.

0 comments:

Post a Comment

Page viewers